M-PAWA KUWAFIKIA WANANCHI POPOTE WALIPO MTAANI

Baadhi ya Mabalozi wa Vodacom Tanzania wanaoenda kutoa elimu kwa wateja wa kampuni hiyo na wananchi kwa ujumla kuhusiana na huduma ya M-Pawa wakimsikiliza Mkuu wa Mawasiliano na Masoko wa kampuni hiyo,Kelvin Twissa wakati wa uzinduzi wa kampeni ya ‘M-Pawa Tumekufikia’ yenye lengo la kuwaelimisha wateja wake nchi nzima kuhusiana na manufaa ya huduma ya M Pawa inayowawezesha kujiwekea akiba na kujipatia mikopo nafuu kwa urahisi zaidi.Uzinduzi huo ulifanyika makao makuu ya kampuni hiyo Mlimani City jijini Dar e Salaam leo.
Mkuu wa Mawasiliano na Masoko wa Vodacom Tanzania,Kelvin Twissa(wakwanza kushoto)na Ofisa Mkuu wa Idara ya M-Pesa,Jacques Voogt wakizindua kampeni ya ‘M-Pawa Tumekufikia’ yenye lengo la kuwaelimisha wateja wake nchi nzima kuhusiana na manufaa ya huduma ya M Pawa inayowawezesha kujiwekea akiba na kujipatia mikopo nafuu kwa urahisi zaidi.Uzinduzi huo ulifanyika makao makuu ya kampuni hiyo Mlimani City jijini Dar e Salaam leo.
Wateja wa Vodacom Tanzania na wananchi kwa ujumla wanaonufaika na huduma ya M-Pawa inayotolewa na kampuni hiyo kwa kushirikiana na benki ya CBA itawafikia watanzania wengi zaidi baada ya kampuni hiyo kuzindua kampeni ya kabambe ya ‘M-Pawa Tumekufikia’ yenye lengo la kuwaelimisha wateja wake kuhusiana na faida na jinsi ya kunufaika na huduma hii inayowawezesha kujiwekea akiba na kujipatia mikopo nafuu kwa urahisi zaidi.
Kampeni ya M-Pawa tumekufikia ambayo imezinduliwa leo jijini Dar es Saaam itafanyika nchini nzima ambapo wataalamu wa huduma watapita kila mkoa kutoa elimu juu ya matumizi na manufaa yake kwa ajili ya kujikwamua kimaisha. Wanachi wanaoishi mijini na vijijini watapata fursa ya kuelimishwa kuhusu M-Pawa na huduma nyingine za Vodacom Tanzania. Mbali na elimu, wateja watajipatia zawadi mbalimbali na kupata burudani kabambe kutoka kwa wasanii nguli wa hapa nchini.
M-Pawa ni huduma inayowawezesha wateja wa Vodacom M-Pesa kuweka akiba na kupata mikopo kupitia simu zao ambapo sasa imeboreshwa ili kuwawezesha wateja wengi zaidi kupata mikopo. Tangu ilipozinduliwa mwaka jana, huduma hii inazidi kupata mafanikio makubwa ambapo idadi kubwa ya watanzania wanazidi kuichangamkia na kuboresha maisha yao kupitia mikopo yenye masharti nafuu zaidi.
Mkuu wa Mawasiliano na Masoko wa Vodacom Tanzania, Kelvin Twissa amesema katika kipindi cha mwaka mmoja tangu huduma hii ianzishwe imeonyesha kuwa na mafanikio makubwa kwa kuwa tayari wananchi wengi wanazidi kujiwekea akiba na kujipatia mikopo inayowawezesha kukabiliana na dharura na kujikwamua kiuchumi kwa njia rahisi ya kupitia simu zao za mkononi.
"Kadri siku zinavyozidi kusonga mbele, wananchi wengi wamezidi kuipokea huduma hii zaidi ya matarajio yetu. Watu wengi wamshafungua akaunti za M-Pawa, wengi wanazidi kujiunga kila kukicha na wengi wanafurahia mikopo kupitia huduma hii. Mpaka sasa zaidi ya wateja milioni mbili wanatumia M-Pawa na tunawakaribisha wote kujitokeza katika kipindi cha kampeni hii kupata ufahamu zaidi. Ratiba za misafara ya watoa elimu hii kwenye maeneo mbalimbali zitakuwa zikitolewa kwenye vyombo vya habari hususani redio kwenye maeneo husika”.
Alisema teknolojia hii ya M-Pawa au “kibubu” ni mkombozi kwa wananchi wengi wa Tanzania ambao walikuwa hawajafungua akaunti za benki “Kuna wananchi wengi wamekuwa na utaratibu wa kukaa na fedha nje ya mabenki, ambako hazileti riba zinawekwa kwenye magodoro,wengine kuzichimbia ardhini na darini,fedha hizi haziko salama ni bora kuziweka M-Pawa” anasema Twissa.
Kuhusu jinsi gani ya kutumia huduma hii mpya ya M-pawa, Twissa, alisema ni rahisi, mteja haitaji kutuma wala kujaza fomu za maombi. Kila mmoja sasa anaweza kufungua akaunti ya benki kwenye benki ya CBA kwa urahisi zaidi kiasi tu cha kuchagua M-Pawa kutoka simu yake ya mkononi katika menu ya huduma ya M-Pesa. Zaidi, haina gharama zozote wala ukomo wa kutoa ama kuhamisha fedha kutoka M-pesa kwenda M-pawa na kinyume chake.
Aliwataka watanzania kuchangamkia fursa hii na kupata elimu ya mikopo, akiba na riba kutoka M-Pawa “Watanzania wengi bado hawana akaunti za benki na sifa za kukopesheka kutoka taasisi za fedha. M-Pawa ni mkombozi kwa wanyonge na wajasiriamali kwani inawawezesha kujiwekea akiba na kupata mikopo isiyo na masharti magumu”.Alisisitiza.

No comments:

Post a Comment

Pages