SERIKALI YAIPONGEA BENKI YA ACCESS KUFUNGUA TAWI LAKE JIJINI MBEYA



Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Abbas Kandoro akizungumza na wateja pamoja na wafanyakazi wa Benki ya Access wakati alipokuwa mgeni rasmi katika sherehe za uzinduzi wa tawi la benki hiyo jijini Mbeya mwishoni wa wiki iliyopita. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Mhe. Dk. Norman Sigallah King na kutoka kushoto ni Ofisa Masoko Mwandamizi wa Access Bank, Jonas Muganyizi Bisheko, Meneja wa Mkoa wa Benki ya Access Mbeya, Emmanuel Venance na Mwakilishi wa Benki ya Access kutoka Makao makuu jijini Dar es salaam, Sebastian Gaissert. 
(PICHA ZOTE NA CATHBERT ANGELO KAJUNA WA KAJUNASON BLOG-MBEYA).
Mwakilishi wa Benki ya Access kutoka Makao makuu jijini Dar es salaam, Sebastian Gaissert, akitoa hotuba yake katika sherehe za uzinduzi wa tawi la benki hiyo mkoani Mbeya.

Meneja wa Mkoa wa Benki ya Access Mbeya, Emmanuel Venance akizungumza machache wakati wa sherehe za uzinduzi wa tawi la benki hiyo mkoani Mbeya.

Wafanyakazi na wageni walioalikwa waliohudhuria sherehe za uzinduzi wa tawi la benki hiyo mkoani Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Abbas Kandoro akikata utepe kuashiria kuzinduliwa rasmi kwa Benki ya Access tawi la Mbeya. Pembeni kulia ni Ofisa Masoko Mwandamizi wa Access Bank, Jonas Muganyizi Bisheko na Mwakilishi wa Benki ya Access kutoka Makao makuu jijini Dar es salaam, Sebastian Gaissert.
Akiweka na jiwe la Msingi...

Meneja wa Tawi la Benki ya Access- Mbeya, Makange Kilimali akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Abbas Kandoro mara baada ya kuingia ndani ya Benki hiyo.

Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya ya Mbeya wakifungua akaunti katika Benki ya Access baada ya kuzinduliwa rasmi.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Abbas Kandoro akionyesha kitambulisho chake mara baada ya kufungua akaunti katika benki hiyo.
Viongozi wakiwa katika picha na Mkuu wa Mkoa, Mh. Abbas Kandoro (wa pili toka kulia) pembeni yake ni Mkuu wa Wiyala ya Mbeya, Mhe. Mhe. Dk. Norman Sigallah King na Ofisa Masoko Mwandamizi wa Access Bank, Jonas Muganyizi Bisheko. Wengine toka kushoto ni Meneja wa Tawi la Benki ya Access- Mbeya, Makange Kilimali, Meneja wa Mkoa wa Benki ya Access Mbeya, Emmanuel Venance na Mwakilishi wa Benki ya Access kutoka Makao makuu jijini Dar es salaam, Sebastian Gaissert.
Wafanyakazi wakiwa katika picha ya pamoja na mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya.
---

*WANANCHI WAMETAKIWA KUITUMIA KUPATA MIKOPO.

Na Mwandishi Wetu, Mbeya.
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, amewataka wakazi wa jiji la Mbeya kuacha kasumba ya kuhifadhi fedha nje ya mfumo wa kibenki kwa kuwa unadidimiza ukuaji wa kiuchumi.
Kandoro aliyasema hayo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati alipokuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa tawi la Benki ya Access katika hafla iliyofanyika kwenye viunga vya tawi hilo Mafiati jijini Mbeya.
Alisema katika utafiti uliofanyika mwaka 2013 ulibaini kuwa ni asilimia 7 tu ya wakazi wa Mkoa wa Mbeya ambao hutumia mifumo ya kibenki kuhifadhi fedha zao huku asilimia 93 wakihifadhi majumbani mwao.
Alisema tabia ya kuhifadhi fedha majumbani haisadii katika kuongeza mzunguko wa fedha bali huchangia kudidimiza uchumi wa Mkoa kutokana na fedha hizo kutoingia kwenye mzunguko wa soko.
Aliongeza kuwa kitendo cha kuhifadhi fedha majumbani pia huchangia kuwavutia majambazi ambao huweza kuvamia na kuiba hivyo njia pekee ya kuhifadhi fedha ni kwa njia ya benki.
Aidha Mkuu wa Mkoa alitoa wito kwa watumishi wa benki kufanya kazi kwa uadilifu na kuwa waaminifu kwa wateja wao kwa kuepuka kuiba fedha kwenye akaunti zao pamoja na kuvujisha siri za ndani za akaunti ya Mteja.
“ Ni toe wito kwa watumishi epukeni kuvujisha siri za akaunti za wateja wenu, wizi kwa njia za mtandao hivyo jengeni imani kwa wananchi kwa kufanya kazi kwa uadilifu” alisema Kandoro.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Benki hiyo kutoka Makao makuu Dar es salaam, Sebastian Gaissert, Benki hiyo imevutiwa kufungua tawi mkoani Mbeya kutokana na kuwa miongoni mwa Mikoa yenye shughuli nyingi za kiuchumi na inayokua kwa kasi kimaendeleo.
Alisema sababu nyingine ya kufungua tawi Mkoa wa Mbeya ni kutokana na kuiunganisha Tanzania na nchi jirani hivyo kuchochea shughuli za kibiashara pamoja na kuwa tegemeo kwa kilimo cha mazao ya chakula na biashara.
Aliongeza kuwa sababu ya pekee ni kuimarika kwa ulinzi na usalama hivyo kuipelekea benki hiyo kuvutiwa na hali hiyo na kuona ni sehemu salama kwa ajili ya uwekezaji mkubwa.
Alisema tangu kufunguliwa kwa Tawi hilo Mkoani Mbeya Januari Mwaka huu zaidi ya mikopo 600 yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 1.5 imetolewa kwa wateja wao pamoja na kufanikiwa kufungua akaunti mpya zaidi ya 1500.

No comments:

Post a Comment

Pages