VALENTINE LOVERS' DINNER AND TALK - MBEZI GARDEN HOTEL: 14.02.2015


Imekuwa ni kitu cha kawaida kwa wapendanao kusherehekea na kufurahi pamoja siku ya Valentine tar 14.02.2015 kila mwaka, sio kwamba nyakati nyingine wapendanao hawana nafasi za kuonyesha mapenzi yao, la hasha, utofauti ni kwamba siku hii inakuwa na hamasa na bashasha zaidi, na wengi kujitokeza kuonyesha kitu cha tofauti kwa wapenzi wao. Inawezekana sana ukasherehekea, ukafurahia, kula na kunywa na mwisho wa siku mahusiano yako na mpenzi wako yakabakia vile vile yalivyokuwa, hapa tunakuja na fursa njema kwako, kuyaruhusu mahusiano yako kupevuka na kukua zaidi kwa kujifunza mambo yatakayoboresha kuhusiana kwenu wakati huo huo mkila, mkinywa na kufurahi. Tunakuletea VALENTINE LOVERS' DINNER & TALK itakayofanyika siku ya Jumamosi tar 14.2.2015 pale Mbezi Garden Hotel, Mbezi Beach kuanzia saa moja jioni. Kwa moyo mkunjufu kabisa napenda kuwaweka mbele yako partners waliosimama pamoja kuhakikisha tukio hili linakufikia. Shukrani za pekee sana ziwafikie

 Christom Solution ni kampuni inayojishuhulisha na kuandaa, kupanga na kuratibisha matukio ya kijamii, kiserikali na shuhuli za makampuni "Corporate events". Christom solution wanajishuhulisha  pia na ushauri wa kisaikolojia "Counselling therapy" pamoja na mafundisho na mazungumzo ya halaiki katika kuhamasisha na kutia moyo "Public, inspirational and motivational talks". Kwa kupata huduma zao wasiliana nao kwa namba 0713 407182 au chrismauki57@gmail.com

  Sherehe yetu ni blog maarufu sana hapa nchini kwa sasa inayokuwezesha kupata kila unachohitaji kuhusu styles za shuhuli kama maharusi, sendoff, kitchen poarties na nyingine nyingi, za ndani ya nchi na nje ya nchi. Baadhi ya picha unazoziona ndani ya www.chrismauki.com ni vionjo tu, picha nyingi zaidi utakutana nazo kwenye www.shereheyetu.com. Hawa wanashiriki pia katika kulitangaza tukio hili la wapendanao

 Siku hiyo wapendanao waliodumu katika mahusiano kwa muda mrefu zaidi na wale ambao ndio wapya zaidi kwenye mahusiano watatuwakilisha kukata keki maalumu iliyotolewa kwa hisani kubwa ya Angela Cakes. Katika shuhuli mbali mbali, kwa mahitaji ya keki za aina zote wasiliana na Angela Cakes kwa 0782 297408.
 Usisahau kabisa kwamba siku ya wapendanao ndio ile miziki na nyimbo za taratiiibu za mapenzi na jumbe za kuhamasisha mahusiano zitayafikia masikio yako kupitia spika murua kutoka Respect DJ's. Hawa wanasimama thabiti kuhakikisha mahitaji yako yote ya muziki na PA System yanakamilika. Sikuhiyo DJ mix zote na Sound system itamilikiwa na Respect DJ's. Red carpet pia ita nakshiwa na vijana wa Respect DJ's. Shukrani za dhati zikufikie mpiganaji wangu Abdul Kimanga.


 Mambo ya kupendeza na kutoka fresh na kitanashati yana wenyewe. Nakuletea mbele yako wenye shuhuli hii ya kuhakikisha unatokelezea na unasimama smart pale kati. Ni RM Collections. Hawa wanahusika zaidi na uuzaji wa suti za kiume, viatu, miwani za ukweli na za kisasa kabisa kutoka nchi mbalimbali, wana nguo za kike pia, wana blazers "makoti ya juu ya wanaume", hizi ni za ukweli sanaaaa, wana tai za rangi na material tofauti. Wanapatikana Migombani street kwenye kona ukitokea Hospitali ya Kairuki kama unapita njia ya kutokea Shoppers Plaza, au njia ya kwenda Ursino street. Ukitokea Shoppers duka lipo kushoto hapo hapo kwenye kona na ukitokea Kairuki hospital duka lipo kulia kwako kwenye kona utaona bango kubwa juu ya duka RM Collections. Wacheki kwa namba 0767 224 504. RM Collection watasimamia kiuthabiti zoezi la kuhakikisha mzungumzaji wa valentine talk anapendeza kuanzia chini hadi juu. Shukrani za dhati na za kipekee ziwafikie RM Collections

No comments:

Post a Comment

Pages