WASHINDI AIRTEL YATOSHA ZAIDI WAKABIDHIWA MAGARI


Mkurugenzi wa masoko wa Airtel bw. Levi Nyakundi (kushoto) akimkabidhi mmoja kati ya washindi wa promosheni ya Yatosha Zaidi bi. Mwajabu Omary katika makabidhiano yaliyofanyika katika ofisi za makao makuu ya Airtel Tanzania. Anayeshuhudia (katikati) Mkurugenzi wa wa kitengo cha Mawasiliano bi Beatrice Singano Mallaya .Airtel imekabidhi magari matatu katika hafla hiyo.
KAMPUNI Ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania asubuhi imekabidhi magari kwa washindi watatu wa kwanza wa promoseni ya Yatosha Zaidi.

Hafla hiyo fupi ya kuvutia ilifanyika Makao Makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na waandishi wa habari, wafanyakazi wa Airtel na wageni waalikwa kadhaa.

Mkurugenzi wa Masoko wa Airtel Levi Nyakundi aliwaomba washindi kuendelea kutumia mtandao wa Airtel kwani kwa sasa wao ni sehemu ya familia ya kampuni hiyo.

Washindi hao ni mkazi wa mkoani Pwani, Ramadhan Dilunga (53) ambaye ni mkulima, mwalimu mstaafu na anayeishi Mtwara, Namtapika Kilumba (60) na mfanyabiashara mkazi wa Dar es Salaam, Mwajabu Churian (27).

Akizungumza kwenye hafla hiyo, Mkurugenzi Mawasiliano Bi Beatrice Singa Mallya  alisema: “Tukio hili la leo linaweza kuchukuliwa kama mwanzo wa mipango mingi iliyopo kwenye kampuni yetu. Kuna mambo mengi yanakuja na madhumuni yetu makubwa ni kushiriki katika kubadilisha na kuboresha maisha ya Watanzania kadhaa wenye bahati.

“Tunaridhishwa na kufurahia uungwaji mkono tunaoupata kutoka kwa wateja wetu, vyombo vya habari na pia serikalini, ieleweke kwamba Airtel ipo na itaendelea kuwapo nchini.”

Akizungumza kwa niaba ya washindi wenzanke Mwajabu Omary alisema: “Tunachoahidi kwa uongozi wa Airtel na wafanyakazi wake ni kwamba, tutaendelea kuunga mkono huduma zinazotolewa na Airtel. Kwa ushindi wetu huu si ndugu na jamaa zetu pekee ndio watatiwa moyo wa ushiriki kwenye promesheni ya Airtel Yatosha Zaidi, bali pia Watanzania wote.”

Wiki moja iliyopita, Airtel Tanzania ilizindua promosheni ya Airtel Yatosha Zaidi Promotion kwa kutenga magari 60 mapya aina ya Toyota IST kama zawadi kwa washindi. Kila siku kwa siku 60 gari moja litatolewa kwa mteja atakayeshinda.

Wikiendi iliyopita, washinda hawa waliozawadiwa magari leo walitangazwa baada ya droo kufanyika. Droo hiyo ilishuhudiwa na mwakilishi kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha huku Balozi wa Airtel Yatosha, msanii wa filamu, Elizabeth Michael maarufu zaidi kama Lulu, akiwatangaza washindi.

No comments:

Post a Comment

Pages