Kongamano la Diaspora na Wajasiriamali likiendelea kwa siku ya pili jijini Dar es Salaam

Chukwu-Emeka Chikezie akiongoza moja ya mdahalo katika kongamano la Diaspora, Balozi wa Marekani nchini Mhe. Mark Childress kwa pamoja na Bw. Ali Mufuruki, Mwenyekiti wa Jumuiya ya Maafisa Watendaji Wakuu nchini, Bw. Richard Miles, Mwakilishi wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Marekani nchini na Dkt. Silencer Mapuranga, Mchumi kutoka ITC.
Balozi wa Marekani nchini, mhe. Childress akichangia mada kuhusu mabadiliko ya kiuchumi Tanzania wakati wa Kongamano la Diaspora.
Bw. Miles nae akichangia wakati wa mjadala kuhusu mabadiliko ya kiuchumi nchini Tanzania na namna ya kuwashirikisha wafanyabiashara wadogo na wakati katika maendeleo ya nchi.
Balozi Mulamula akizungumza wakati wa mjadala huo .
Balozi wa China nchini, Mhe. Lu Youqing akiwasilisha mada kuhusu Mapinduzi ya Viwanda nchini na wajibu wa Diaspora katika ukuaji wa SME's
Balozi Lu akiwasilisha mada yake
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula kwa pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Uswisi, Mhe. Modest Mero wakimsikiliza Balozi wa China nchini (hayupo pichani) wakati akiwasilisha mada
Washiriki wakifuatilia mada kutoka kwa Balozi wa China
Balozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Mhe. Hemed Mgaza akiwa na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Diplomasia, Dkt. Bernard Achiula wakisikiliza kwa makini uwasilishwaji wa mada wakati wa kongamano la Pili la Diaspora.
Mada zikitolewa
Maafisa Mambo ya Nje wakijadili jambo 
Timu ya Waandishi wa kumbukumbu za mkutano kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakinukuu taarifa mbalimbali wakati wa Kongamano la Diaspora ili kuweka kumbukumbu za tukio hilo sawasawa
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bibi Rosemary Jairo akizungumza wakati wa kongamano hilo
Mada zikiendelea kutolewa wakati wa kongamano hilo 
Washiriki wa kongamano .Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Pages