Meneja
Uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando akiongea na waandishi wa habari kusiana
na huduma mpya ya linda simu ya Airtel Simu Bima itakayowasaidia wateja wote
wanaotumia Simu za Smartphone kuziwekea Bima simu zao na kulipia kupitia huduma
ya Airtel Money, kulia ni Meneja wa Airtel Money Bw, Moses Alphonce na kushoto
ni Muwakilishi wa shirika la Bima la UAP bw, Charles Matondane.
 Meneja
Masoko wa kampuni ya Bima ya UAP bw, Raymond Komanga akielezea jinsi mfumo wa
malipo wa Airtel SimuBima unavyofanya kazi kwa kushirikiana  kampuni yake mara baada ya uzinduzi wa huduma hiyo
ya kulinda simu za smartphone kupitia bima ijulikanayo kama Airtel SimuBima,
katikati ni Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando na Meneja wa Airtel Money
bw, Moses Alphonce (kulia) huduma ya AirtelSimuBima itawawezesha wateja wa
Airtel pamoja na watumiaji wote wa Smartphone nchini kuepuka hasara pale simu
inapopotea au kuibiwa.

 
Toka
kulia ni meneja wa Airtel Money bw, Moses Alphonce akiwa na Meneja Uhusiano wa
Airtel Jackson Mmbando wakionyesha jinsi huduma yao ya kulipia simu za
smartphone Bima ijulikanayo kama  “Linda simu
na Airtel Simu Bima” Inavyofanya kazi. Kupitia huduma hiyo sasa wateja wote
wanaotumia Smarphone nchni wataweza kuziwekea Bima zao simu  kulipia kupitia huduma ya Airtel Money na
endapo simu hiyo itaibwa au kupotea mteja atalipwa ndani ya siku tano. kushoto
anaefuatilia uzinduzi huo ni muwakilishi wa kampuni ya bima ya UAP Tanzaninia bw
Charles Matondane ambao wao watakuwa wakiwalipa wateja.
Na Mwandishi Wetu,
·        Wateja wa mitandao mingine pia wataweza kusajili simu zao na bima hiyo na kulipia kwa Airtel money
·        Airtel Simu Bima kufidia simu za wateja wake zilizopotea au kuibwa
Kampuni
 ya simu za mkononi Airtel kwa kushirikiana na kampuni ya Bima ya UAP 
leo wamezindua huduma kabambe itakayowasaidia wateja wote wanaotumia 
Simu za Smartphone kuziwekea Bima simu zao na kulipia kupitia huduma ya 
Airtel Money. 
Huduma hiyo mpya nchini kwa watumiaji wa smartphone itajulikana kama “Airtel SimuBima”
 ambapo itawawezesha wateja wa Airtel pamoja na watumiaji wote wa 
Smartphone nchini kuepuka hasara pale simu inapopotea au kuibiwa.
Akiongea
 wakati wa uzinduzi huo Meneja Uhusiano wa Airtel Tanzania Jackson 
Mmbandoalisema “Leo Airtel tumeongeza sababu nyingine kwa wateja wetu 
kuendelea kufurahia huduma zetu, sasa wateja wote wenye simu orijino za 
smartphone wataweza kusajiliwa na huduma ya ‘Airtel SimuBima’ ambapo mteja
 mmoja anataweza kusajili hadi simu mbili  katika mfumo huu. Ikitokea 
mteja ameibiwa simu yake au kuipoteza basi kupitia huduma hii ya ‘Airtel SimuBima’ tutampatia
 mteja huyo pesa ili aweze kununua simu nyingine atakayotaka na kisha 
simu iliyopotea itazimwa moja kwa moja isiweze kutumika tena”.
“Mteja wa Airtel ataweza kufaidi huduma ya “Airtel SimuBima”
 mara baada ya kupakuwa aplikesheni ya simuBima kutoka kwenye Playstore 
na kusajili taarifa za smartphone yake ikiwemo IMEI namba pamoja na 
gharama ya simu yake  na papohapo atapata ujumbe utakaomwambia gharama 
ya Bima ya simu hiyo kwa mwaka ambayo ataamua kuilipa yote au kuwa 
anailipa kwa kila mwezi” aliongeza Mmbando 
“Airtel Tanzania tunaamini kuwa ushirika wetu na shirika la bima la UAP kupitia ‘Airtel SimuBima’ utasaidia
 kuhamasisha watumiaji wa simu za mkononi kununua simu orijino ili 
waweze kufurahia huduma hii pamoja na huduma zingine za Airtel za 
kimtandao kama vile Airtel TV, Kujisomea masomo ya VETA –VSOMO kupitia 
mtandao pamoja na kufaidi aplikesheni mbalimbali za airtel zenye 
kusaidia wateja katika mambo ya kiuchumi na kijamii” alieleza Mmbando
Kwa
 upande wake Mkurugenzi wa UAP Bw, Raymond Komanga alisema 
“tunawahakikishia wateja wote wa Airtel watakaosajili namba zao katika 
huduma ya Airtel SimuBima kwamba tutawalipa madai yao haraka sana pale 
wanapopatwa na tatizo la kupoteza simu au kuibiwa simu zilizowekewa Bima
 ndani ya siku tano tu tokea pale wanapotoa taarifa kituo cha polisi na 
kutujulisha sisi, tutalipa simu za hadi shilingi milioni moja na laki 
tano, lakini wateja waelewe kuwa bima yetu haitakuwa ikilipa simu 
kuvunjika au 
Komanga aliendelea kuelezea kuwa “Ikitokea simu ya mteja iliyosajiliwa na “Airtel SimuBima”
 imepotea au kuibiwa mteja atatakiwa kutoa taarifa mapema sana na kupata
 taarifa ya polisi kuhusiana na upotevu huo au wizi ili kuweza 
kukamilisha malipo yake. Swala hili linatakiwa kufanywa na wateja wote 
waliojisali na kulipia bima ya mwezi au ya mwaka mzima kupitia  Airtel 
SimuBima” 
Wateja wa “Airtel SimuBima”
 wataweza kudai malipo yao kwa kutumia simu nyingine ya smartphone na 
kuingia katika Aplikesheni ya Airtel SimuBima kisha kufuata maelekezo ya
 malipo. Vilevile mteja anaweza kutumia kompyuta na kuingia katika 
ukurasa wa ‘Airtel SimuBima’ na kukamilisha taarifa za madai.
“Ukitaka kulipia huduma hii ya ‘Airtel SimuBima’ piga *150*60# kisha chagua malipo, na uchague SimuBima, papohapo malipo yatatufikia sisi moja kwa moja”.  Bw, Komanga alisema.
 
0 Comments