DKT. PHILIP MPANGO ABAINI BAADHI YA WAFANYABIASHARA DODOMA HAWATUMII IPASAVYO EFDs






Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akikagua mashine ya EFD na risiti ya kieletroniki aliyopewa baada ya kununua bidhaa kwenye moja ya maduka mjini Dodoma, alipofanya ziara ya kushitukiza kukagua kama wafanyabiashara wa mji huo wanatumia ipasavyo mashine hizo.

Kiongozi wa Timu Maalumu ya Ukaguzi wa Mashine za EFD’s kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani Dodoma, Bw. Godfrey Patrick (wa pili kushoto) akifafanua jambo wakati wa ziara ya kushitukiza iliyofanywa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), kwenye maduka mjini Dodoma.

Mfanyabiashara wa duka la rejareja mjini Dodoma, Bw. Donald Chami, akimwonesha mashine ya kieletroniki ambayo imeharibika, Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), baada ya kufanyaziara ya kushitukiza kwenye duka lake na kubaini kuwa hatoi risiti za kielektroniki kwa wateja wake.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akipitia kwa makini fomu ya makadirio ya kodi iliyotolewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika moja ya duka la vipodozi mjini Dodoma wakati alipofanya ukaguzi wa matumizi ya mashine za EFD’s katika baadhi ya maduka yaliyopo mjini humo.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akimuonya mfanyabishara wa mjini Dodoma, Bw. Isdori Shirima, baada ya kukuta akiuza bidhaa bila kutoa risiti za kielektroniki kwa wateja wake inavyotakiwa na kuagiza Mamlaka ya Mapato mkoani humo kufanya ukaguzi wa kina ili kubaini kiwango cha ukwepaji kodi cha mfanyabiashara huyo na kumchukulia hatua za kisheria.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akikagua risiti ya mteja aliyenunua tanki la kuhifadhia maji katika moja ya duka linalouza vifaa vya ujenzi mjini Dodoma, na kutoa wito kwa wananchi kukagua risiti zao ili kubaini kama kiwango kilichoandikwa kinalingana na kiasi kilichoandikwa kwenye risiti.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akimwelekeza mwananke mmoja aliyemkuta dukani akague risiti yake baada ya kufanya manunuzi kwenye duka moja la vifaa vya ujenzi mjini Dodoma, alipofanyaziara ya kushitukiza ili kubaini namna wafanyabiashara wa maduka mjini humo wanavyotumia mashine za kielektroniki za kutolea risiti.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akimuagiza Meneja Msaidizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani Dodoma, Bw. Ngaka Magere, kumkutanisha na mawakala wanaosambaza mashine za kieletroniki za kutolea risiti mkoani humo baada ya kutoridhishwa na huduma zao.

Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Mb), akisikiliza maelezo ya matumizi ya mashine za kielektroniki kutoka kwa mfanyakazi wa Kituo kimoja cha Mafuta mjini Dodoma, alipofanyaziara ya kushitukiza kituoni hapo kuangalia matumizi ya mashine hizo.

Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) akikagua risiti na kupata maelezo kutoka kwa mhudumu wa Kituo cha Mafuta cha ORYX mjini Dodoma, Bi. Hanifa Shaldin, alipofanya ziara ya kushitukiza kuangalia kama vituo vya mafuta mjini humo vimefungwa mashine za kielektroniki za kutolea risiti kwa wateja wao. (Picha zote na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-WFM).

No comments:

Post a Comment

Pages