Usiku wa Old is Gold taarab kila Jumapili ndani ya Safari Carnival
Na Andrew Chale
USIKU
wa Old is Gold taarab unatarajiwa kurindima ndani ya ukumbi wa Safari
Carnival, Mikochezni B, kwa wadau kupata burudani ya muziki wa mwambao
wa kizamani.
Kwa
mujibu wa waandaji wa usiku huo, Mkurugenzi wa Fabak Fashions, Asia
Idarous Khamsin alieleza kuwa ni kila Jumapili ndani ya ukumbi huo
utakuwa na burudani ya kipekee kwa nyimbo za mwambao pamoja na
‘surprise’ mbalimbali kwa watakaofika hapo.
“Kila
jumapili kwa kiingilio cha sh 5,000 tu. Wapenzi wa muziki wa
mwambao watashuhudia shoo ya Usiku wa Old is Gold ndani ya Safari
Carnival” Alisema Asia Idarous
Aliongeza
kuwa, mbali na burudani ya taarab za zamani pia kutakuwa na ‘Surprise’
mbalimbali" kwa wadau watakaojitokeza kwenye usiku huo.
Aidha, Asia Idarous alisema usiku huo, pia umedhaminiwa na Safari Carnival, Fabak fashions, Clouds fm, Gone Media, Maji Poa, Michuzi Media Group na wengineo.
No comments:
Post a Comment