Mkuu
wa Masoko na Mawasiliano wa Vodacom, Kelvin Twissa(katikati)akiongea na
waandishi wa habari hivi karibuni (hawapo pichani)wakati wa uzinduzi wa
Promosheni ya JayMillions,Wengine katika picha kushoto ni Balozi wa
Promosheni hiyo Hilary Daud”Zembwela” na kulia ni Meneja Uhusiano wa
kampuni hiyo Matina Nkurlu.
Uwezo
Magendege, 22, ni mshindi wa kwanza wa zawadi nono ya siku ya pesa
taslimu Sh. 100m/- za promosheni iliyozinduliwa siku 19 zilizopita na
kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom Tanzania.
Hadi
kufikia leo ni Sh. 126m/- pekee zilizokwisha kuchukuliwa na Uwezo,
washindi wengine wawili – Hyness Petro Kanumba from Rukwa and James
Mangu (Mwanza) – wa Sh. 10m/- na sita – Chiliphod Wanjala (Mwanza),
Janeth Ngannyange (Njombe), Evarista A (Mwanza), Stanley Bagashe
(Shinyanga), Ramadhani H. Maulid (Dodoma) and Lucas M (Shinyanga) – wa
Sh. 1m/-. Kiasi cha zaidi ya Sh. 5bn/- (ambazo ni sawasawa na magari
madogo 428 ya muundo wa mgongo wa kobe) zingeweza kunyakuliwa na wateja
iwapo wangetuma neno “JAY” kwenda 15544 kucheki kama wameshinda.
Uwezo
ni mkazi wa wilaya ya Kilolo, mkoani Iringa. Mnamo Alhamis Januari 29,
2015, Uwezo alipokea simu ambayo ilipelekea maisha yake kubadilika
milele alipotaarifiwa kuwa amejishindia Sh. 100m/- kutoka katika
mamilioni ya shilingi yanayogawiwa kupitia promosheni ya JayMillions ya
Vodacom Tanzania kwa siku hiyo.
“Nawasihi
wateja wote wa Vodacom wasiache kucheki kila siku kujua kama
wameshinda. Mimi ndoto zangu zinatimia kupitia promosheni hii maana
tangu kuanzishwa kwa JayMillions nimekuwa nikicheki kila siku. Pamoja na
kupata ujumbe kwamba sijashinda mara kila mara, sikuacha kucheza. Siku
ile nilipoamua kutuma “AUTO” kwenda 15544 ndipo nilipopata ujumbe papo
hapo kwamba nimeshinda,” alielezea Uwezo, akiwa na furaha tele.
Uwezo
anategemea kutumia sehemu ya pesa alizoshinda kujilipia ada ya shule
ambapo amepanga kujiunga na mkondo wa biashara katika elimu ya juu.
Amepanga pia kuwekeza sehemu ya mapato haya katika mradi wa upandaji
miti. Kwake yeye mradi huu si tu sehemu ya kujipatia kipato bali utakuwa
ni kumbukumbu ya bahati hii aliyopata kwa vizazi vyake vijavyo.
Promosheni
ya JayMillions ni ya kipekee nchini ambapo kila siku wateja wote wa
Vodacom huingizwa kwenye droo halafu wateja 111 huchaguliwa ambapo
wanaweza kujishindia zawadi za pesa taslimu iwapo watacheki.
Kila
siku mteja mmoja wa Vodacom anaweza kujinyakulia kitita cha Sh. 100m/-,
wateja 10 kujishindia Sh. 10m/- na wateja 100 kujishindia Sh. 1m/-.
Wateja 10,000 wanaweza kujishindia muda wa maongezi wenye thamani ya Sh.
1000/- kila siku. Kujua kama wameshinda, wateja wa Vodacom wanapaswa
kucheki kila siku kwa kutuma neno “JAY” kwenda 15544.
“Tunaendelea
kuwasisitizia wateja wetu wacheki kila siku ili kujua kama namba zao
zimeshinda. Kama Uwezo asingetuma ujumbe siku ile angeendelea tu na
maisha yake kama yalivyokuwa bila kujua kama namba yake ilichaguliwa
kushinda. Hadi hivi sasa tuna washindi 9 wa zawadi za pesa taslimu Sh.
126m/- lakini kila siku wateja 111 wanachaguliwa kushinda. Bado kuna Sh.
24.3bn/- za kushindaniwa kwa siku 81 zilizosalia kwenye promosheni hii
hivyo endeleeni kutuma “JAY” kwenda 15544 kila siku,” alisema Mkuu wa
Masoko na Mawasiliano wa Vodacom, Kelvin Twissa.
Baada
ya kutuma neno “JAY” kwenda 15544, mteja atapokea ujumbe kumjulisha kama
ameshinda au la. Kama hajashinda atashauriwa kujaribu tena siku
inayofuata. Kila ujumbe mfupi unagharimu Sh.300/- lakini tofauti na
promosheni zilizopita, JayMillions haina maswali mengi, wala chemsha
bongo. Kila mteja ana nafasi ya kushinda.
0 Comments