WASHIRIKI WA MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2015 WAHIMIZA WANAKIJIJI KUFANYA KILIMO CHA BIASHARA, WAWAPA BURUDANI WANAKIJIJI


 Hapa ilikuwa ni mapema kabisa ambapo washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula msimu wa Nne wakiwa wanajikusanya kwa ajili ya kupewa mwongozo wa siku nzima
 Baada ya washiriki wa Shindano la Mama shujaa wa Chakula  Shindano linalo endeshwa na Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow na kudhaminiwa na Gates and Melinda Foundation,TBS, Cooperative Bank Great Britain na Care Tanzania, baada ya  kuwasili wote sasa wanapangwa makundi makundi kwa ajili ya kuanza mchakato wa siku
 Hapa katika kundi la kwanza washiriki wa Shindano la  Mama Shujaa wa Chakula , Shindano linaloendeshwa na Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow hapa wakiwahamasisha wanakijiji cha kisanga kilimo cha Biashara na kubadilishana mawazo kuhusu nyenzo , mazao na tathimini ya mapato na matumizi.
 Kundi la pili wakiendelea kutoa Elimu ya Kilimo kwa Wanakijiji 
 Kundi la tatu wakiendelea kutoa elimu na kubadilishana mawazo na wanakijiji wa kijiji cha Kisanga
 Mmoja wa Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula , Regina kalipi(Katavi)  akiwa ameshikiriwa na washiriki wenzake baada ya kuanguka akisoma Lisara iliyokuwa inahusu kilimo
Katikati ni Winnie Malya Mshiriki kutoka Kilimanjaro akisoma Lisara kwa wanakijiji ambao hawapo Pichani juu ya kilimo.
 Burudani lilianzia hapa ambapo Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula Pili Kashinje(zanzibar, Neema Hilonga (Manyara) na Mandutha kitoeloh 9Singida)  walishiundana vilivyo katika kukimbia lakini Pili aliibuka kuwa Mshindi.
 Burudani ilizidi kuwa Taaamu zaidi ambapa Washiriki wa shindano la  Mama  Shujaa wa Chakula Shindano linaloendeshwa na Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow na kurushwa katika Runinga yako kupitia Chanel ya ITV kuanzia saa 12:30 Jioni na Kurudiwa saa 11:30 asubuhi , hapa ni pata ni kupate ambapo Winnie Mallya(Kilimanjaro) Edna Kiogwe (Dar es salaam) na Severina Mutahyabarwa (Kagera) walishindana vikali kukukimbia wakiwa wamevaa magunia haa hivyo mshiriki kutoka Kilimanjaro aliwatoa nje na kuibuka mshindi.
 Mambo yalizidi noga zaidi ambapo washiriki waliendelea kutoa Burudaani ya nguvu kwa wanakijiji wa Kijiji cha Kisanga ambapo hapa sasa  Caroline Chilele(Morogoro) , Eva Daudi (Pwani) na Dina Sumari (Meru) walichuna vikari wakiwa wanatembea kwa mwendo wa kasi huku wakiwa na vijiko nyenye ndimu  Mdomoni..Hata hivyo mshindi ilikuwa ni lazima apatikane na Calorine alifanikiwa kuibuka kidedea
 Ulizani washiriki wa shindano la Mama Shujaa wa Chakula hawawezi kuziburuta Njinga.... Ilikuwa ni Burudani zaidi hapa ambapo sasa Hawa Mkata(Mtwara) ,Edna Kiogwe (Dar es salaam), na Upendo Mhomisoli (Njombe)  walishindana vikali kuendesha Baiskeri. Hata hivyo Mshiriki toka Mtwara aliibuka Mshindi
Siku hii kwa hakika wanakijiji walishuhudia Burudani ya kipekee na ya aina yake kabisa, hapa wakina mama hawa walikuwa wanajikumbusha enzi za utoto wao ambapo walicheza ule mchezo Maarufu sana uitwao Reje hapa walidunguana, walitoa kijasho maana shughuli ya kukwepa Mpira si ya masihala, Calorine Chilele(Morogoro) aliibuka Mshindi.
Na Mwisho Washiriki wa Shindano la Mama Shujaa wa Chakula Shindano linaloendeshwa na Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow na kurushwa katika Runinga yako kupitia Chanel ya ITV kuanzia saa 12:30 Jioni na Kurudiwa saa 11:30 asubuhi  ambapo hapa ilikuwa ni vuta ni kuvute mpaka kieleweke hapa washiriki wote walikuwa wanashindana kwa kasi ya ajabu sasa kilichotokea hapa ni cha kushangaza kamba ilikatika hivyo kukawa hakuna mshidi wakatoka sale sale..

No comments:

Post a Comment

Pages