AIRTEL FURSA YAFIKIA VIJANA WILAYANI NGARA

 Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (wa 3 kushoto) akimkabidhi Kanizio Annatory (katikati) ambaye ni miongoni mwa vijana waliowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha” mashine na vifaa vya kuoshea magari pamoja na sehemu ya kisasa ya kufanyia biashara, akishuhudiwa na ndugu zake pamoja na wafanyakazi wa Airtel katika hafla iliyofanyika kijiji cha Kamnazi mkoani Kagera.
 Afisa Uhusiano na matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (kwanza kulia) pamoja na wafanyakazi wa Airtel wakimwonesha Kanizio Annatory (wa pili kushoto)  sehemu ya kisasa ya kuosha magari aliyowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha” baada ya kukabidhiwa mashine na vifaa vya kuosha magari katika hafla iliyofanyika kijiji cha Kamnazi mkoani Kagera.
Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (4 kushoto) akimkabidhi  Kanizio Annatory (2 kulia) ambaye ni miongoni mwa vijana waliowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha” mashine na vifaa vya kuosha gari pamoja na sehemu ya kisasa ya kufanyia biashara, akishuhudiwa na dada yake Agnes Annatory (kulia) pamoja na wafanyakazi wa Airtel katika hafla iliyofanyika kijiji cha Kamnazi mkoani Kagera.
Afisa Uhusiano na Matukio wa Airtel, Dangio Kaniki (wa 3 kushoto) akimkabidhi Kanizio Annatory (katikati) ambaye ni miongoni mwa vijana waliowezeshwa na  mpango wa Airtel Fursa “Tunakuwezesha” mashine na vifaa vya kuoshea magari pamoja na sehemu ya kisasa ya kufanyia biashara, akishuhudiwa na ndugu zake pamoja na wafanyakazi wa Airtel katika hafla iliyofanyika kijiji cha Kamnazi mkoani Kagera.
Mwanzoni mwa wiki hii Airtel kupitia mpango wake wa Airtel Fursa  iliweza kufika  katika  kijiji cha  Kumnazi wilayani Ngara mkoani Kagera  na kumfikia Kijana  Kanizio Annatory anayejishughulisha na   biashara ya kuosha magari, kwa kumpatia vifaa na kufanyiwa ukarabati wa eneo lake la kazi . Vijana wengi wanaamini maisha mazuri na fursa za kiuchumi zinapatikana mjini, lakini kwa Kijana Kanizio kupita kwa barabara katika kijiji hiki ni fursa adhimu kwake.
Airtel Fursa  umelenga katika kuwezesha vijana  wajasiriamali hapa nchini kwa kutoa msaada kwa vijana ambao wanaonyesha juhudi ya kujikomboa na changamoto za maisha katika Jamii zinazowazunguka kwa kuwapatia vitendea kazi na kutoa mafunzo ya biashara ya ujasiriamali. Airtel Fursa ni moja ya sehemu ya utekelezaji wa wajibu wa Airtel  katika kurudisha sehemu ya faida wanayoipata kwa jamii ili kukidhi matakwa ya kiuchumi, na kuunga mkono jitihada za serikali katika kubadilisha maisha ya wananchi.
Akiongea wakati wa makabidhiano afisa uhusiano na matukio wa Airtel, Dangio Kaniki alisema kuwezeshwa kwa kijana huyu  kupitia Airtel fursa ni ukombozi wa kiuchumi kwa familia yake na Jamii inayomzunguka. Kama alivyokuwa amebainisha katika maombi yake kupitia mpango wa Airtel Fursa, hatua hiyo imetafsiriwa kama kichocheo cha mapinduzi ya kibiashara na fursa za kiuchumi kijijini hapa Kumnazi.
“Tunawahimiza vijana kujitokeza kwa wingi na kuchangamkia fursa hizi pale zinapojitokeza kwani baadhi ya vijana  wamekuwa wakihamia  mijini na kuacha kazi ya uzalishaji mali kufanywa na wazee na wanawake  na hivyo kukwamisha  maendeleo vijijini” aliongeza Dangio
Akizungumza mara baada ya kupokea msaada huo, Kanizio amesema msaada huo ni mkombozi wa maisha yake  na familia huku dada yake Agnes Annatory akiishukuru Airtel kwa kuwa mkombozi kwao.
Kanizio alisema “ nawashukuru sana Airtel kwa kuweza kufanikisha ndoto zangu kwa kuweza kunipatia vifaa hivi vya kisasa kwani nimekuwa nikipata ugumu wa kupata wateja kwani sikuwa na vitendea kazi vya kutosha vitakavyoweza kukidhi mahitaji ya wateja wangu, lakini sasa ninaamini nitapata Wateja wengi sana na kuinua biashara yangu.
Mpaka sasa Airtel Fursa toka ianze imeweza kuwainua vijana wapata 2800kwa kuwapatia vifaa mbali mbali kwa kuendeleza bishara zao na vile vile kutoa mafunzo ya biashara katika mikoa mbali mbali hapa nchi, na katika msimu huu wa pili Airtel Fursa imetenga kiasi cha shilingi bilioni moja kwa ajili ya kubadlisha maisha ya vijana hawa.

No comments:

Post a Comment

Pages