BENKI YA DCB WATOA MSAADA WA MADAWATI 100 KATIKA SHULE MPYA YA MSINGI YA LUBAKAYA JIJINI DAR ES SALAAM.


Benki ya DCB COMMERCIAL imetoa madawati 100 kwa shule ya msingi Lubakaya iliyopo Kata ya Zingiziwa jijini Dar es Salaam, ikiwa ni ukamilishaji wa ahadi yake ya kuchangia madawati 300 kwa shule za manispaa tatu za mkoa wa Dar es Salaam.

Mkuu wa kukabiliana na majanga wa Benki ya DCB, Kulwa Deteba akizungumza na waanafunzi pamoja na viongozi mbalimbali jijini Dar es Salaam leo amesema kuwa benki ya DCB imeguswa na tatizo la ukosefu wa madawati kwa shule ya msingi hapa nchini.
Amesema kuwa bodi na uongozi wa benki ya DCB inaunga mkono juhudi za serikali katika kukabiliana na tatizo la madawati hapa nchini inetoa madawati 100 katika shule ya Msingi Lubakaya jijini Dar es Salaam leo.
Nae Mkuu wa shule ya Msingi Lubakaya iliyopo kata ya Zingiziwa, Said Chitumba amewashukueu benki ya DCB kwa mchango wao kwa kutoa madawati 100 katika shule hiyo ikiwa shule hiyo inavyumba 16 vya madarasa na sasa wanaukosefu wa madawati 300.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko akikabidhiwa madawati na Mkuu wa kukabiliana na majanga wa Benki ya DCB, Kulwa Deteba jijini Dar es Salaam leo, madawati ambayo yatapelekwa katika shule Mpya ya Lubakaya iliyopo Kata ya Zingiziwa jijini Dar es Salaam.
  Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko akikabidhiwa madawati na Mkuu wa kukabiliana na majanga wa Benki ya DCB, Kulwa Deteba wakimkabidhi madawati Mkuu wa Shule ya Msingi, Lubakaya (Katikati) jijini Dar es Salaam leo. Katika Hafla iliyofanyika katika Shule ya Msingi Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo.
 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko na Mkuu wa kukabiliana na majanga wa Benki ya DCB, Kulwa Deteba wakiwa wamekaa kwenye madawati mara baada ya kukabidhi madawati kwenye shule ya Msingi Lubakaya iliyopo kata ya Zingiziwa  jijini Dar es Salaam leo.
 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko madawati na Mkuu wa kukabiliana na majanga wa Benki ya DCB, Kulwa Deteba wakiwa wamekaa kwenye madawati na wanafunzi wa shule ya Msingi Mnazi Mmoja wakiwawakilishi wanafunzi wa shule ya Msingi Lubakaya iliyopo kata ya Zingiziwa  jijini Dar es Salaam leo.
   Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko na Mkuu wa kukabiliana na majanga wa Benki ya DCB, Kulwa Deteba wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa shule na wa serikali katika picha ya pamoja mara baada ya kukabidhi madawati 100 kutoka benki ya DCB jijini Dar es Salaam leo.
 Mstahiki Meya wa Manispaa ya Ilala, Charles Kuyeko akizungumza katika Hafla Fupi ya Kuwakabidhi madawati 100 ya  shule ya Msingi Lubakaya iliyopo kata ya Zingiziwa  jijini Dar es Salaam leo.

Mkuu wa shule ya Msingi Lubakaya iliyopo kata ya Zingiziwa, Said Chitumba akiwashukuru Benki ya DCB akiwashukuru benki ya DCB mara baada ya kukabidhiwa madawati 100. 

BENKI YA EXIM YAADHIMISHA MIAKA 19 KWA KUZINDUA HUDUMA TATU MPYA.

Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Benki ya Exim, Selemani Mponda akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kabla ya hafla fupi ya kusherekea miaka 19 ya benki hiyo na kuzindua wa huduma tatu za benki hiyo. Kutoka kushoto ni  Mkuu wa wa Kitengo cha Hatari David Lusala, kulia ni Mkuu wa Rasilimali watu wa benki ya Exim, Fredrick Kanga.
Meneja Operesheni wa Benki ya Exim, Manfredy Kayala akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Kadi za malipo za Exim (TANAPA cards, Master cards and VISA cards) ambazo zinaweza kutumika katika Hifadhi zote za Taifa chini ya TANAPA. Kadi hizi zitaboresha huduma ya malipo ya kielektroniki na pia kuzuia upotevu wa mapato katika tasnia ya Utalii. jijini Dar es Salaam leo. Kushoto ni Mkuu wa Raslimali watu wa benki ya Exim, Fredrick Kanga.
 Mkuu wa Kitengo cha hatari wa Benki ya Exim, David Lusala (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Benki ya Exim, Selemani Mponda na kushoto ni Mkuu wa kitengo cha uhasibu, George Binde.
 Mkuu wa Raslimali watu wa benki ya Exim, Fredrick Kanga akikata utepe kuzindua huduma ya  Mfumo wa kujifunza kupitia mtandao unaoitwa Elimika ambao utaongeza uwezeshaji wa wafanyakazi kwa kiasi kikubwa jijini Dar es Salaam leo.
Mkuu wa Raslimali watu wa benki ya Exim, Fredrick Kanga akionesha bango la huduma ya  Mfumo wa kujifunza kupitia mtandao unaoitwa Elimika ambao utaongeza uwezeshaji wa wafanyakazi kwa kiasi kikubwa jijini Dar es Salaam leo.

Wafanyakazi wa Benki ya Exim wakiwasha mishumaa kwenye keki kusherekea miaka 19 ya benki hiyo hapa nchini jijini Dar es Salaam leo.

BENKI ya Exim Tanzania imesheherekea kuadhimisha miaka 19 ya ukuaji na uvumbuzi kwa kuzindua huduma mpya tatu kwa wateja wake jijini Dar es Salaam leo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mkuu wa Kitengo cha Fedha wa Benki ya Exim, Selemani Mponda amesema kuwa leo wanasherekea miaka 19 tangu kuwepo hapa nchini ikiwa na mafanikio makubwa Katika miaka 19,  benki hiyo imejenga utendaji bora na imara katika fedha wakiwa na rasilimali zenye thamani ya TZS 1.5 Trilioni kufikia Juni 2016. 

Amesema kuwa Faida kabla ya kodi katika kipindi cha pili cha mwaka ilikuwa shilingi bilioni 64 na pia wameweza kuwa na wastani wa ukuaji kwa mwaka wa asilimia 30.

Mafanikio ya benki ya Exim Tanzania ni kuweza kuwa na makao nchini Uganda kwa kununua benki ya Imperial ya Uganda mapema mwaka huu. Benki ya Exim sasa ina hisa za asilimia 58.60 katika taasisi hiyo mpya ambayo inayofanya biashara kama Benki ya Exim Uganda. Wakati ikijikita kuwa benki ya kikanda tayari ina matawi 43 katika nchi nne zikiwemo Tanzania, Uganda, Djibouti na Comoro na pia ikiwa na mipango ya kuendelea kujitanua katika masoko mengine katika miaka mitano ijayo.  

Amesema kuwa huduma zilizozinduliwa ni:-
1. Uwezo wa kutoa taarifa za udanganyifu katika kampeni ya kupambana na udanganyifu ikiwa na lengo la kutengeneza mazingira ya kutokuwa na wizi katika tasnia ya benki.

2.  Kadi za malipo za Exim (TANAPA cards, Master cards and VISA cards) ambazo zinaweza kutumika katika Hifadhi zote za Taifa chini ya TANAPA. Kadi hizi zitaboresha huduma ya malipo ya kielektroniki na pia kuzuia upotevu wa mapato katika tasnia ya Utalii. 

3.   Mfumo wa kujifunza kupitia mtandao unaoitwa Elimika ambao utaongeza uwezeshaji wa wafanyakazi kwa kiasi kikubwa. 

Katika miongo miwili iliyopita, ukuaji wa benki hii na mchango wake wa kiuc humi na kijamii umetambulika sio tu katika Tanzania bali pia katika kanda ya Kusini na Mashariki mwa Afrika kwa sababu ya ubora katika utendaji wake.

No comments:

Post a Comment

Pages