Pamoja
 na kuwepo kwa maendeleo ya kasi katika nyanja mbalimbali lakini sekta 
ya teknolojia inabaki kuwa moja ya njia ambayo imechangia kwa kiasi 
kikubwa kupatikana kwa mafanikio hayo kwa kurahisisha kazi nyingi 
kufanyika kwa haraka.
Kwa
 kutambua hilo, kampuni inayohusika na utoaji wa huduma zinazohusiana na
 teknolojia ya EnGenius imeingia katika makubaliano na kampuni ya 
usambazaji wa vifaa vya kiteknolojia ya Red Dot ili iweze kusambaziwa 
vifaa na huduma mbalimbali ambazo zinafanywa na Red Dot katika nchi za 
Afrika Mashariki.
Mkuu
 wa Kanda wa EnGenius, Van Hsiao akizungumzia kazi ambazo wanazifanya na
 mipango ya kutoa bidhaa bora kwa nchi za Afrika Mashariki.
Kampuni
 ya EnGenius ambayo inatoa huduma kama za internet wireless, radio 
frequency (RF) technology na kusambaza bidhaa mbalimbali kama kompyuta 
imesema kuwa imefanya maamuzi ya kuingi katika makubaliano na Red Dot 
ikiamini kuwa ni moja ya njia sahihi ambayo itawawezesha kuwafikia 
wateja kwa karibu zaidi.
Akizungumzia
 makubaliano hayo, Mkuu wa Kanda wa EnGenius, Van Hsiao alisema kampuni 
ao kwa sasa inahitaji kujitanua katika nchi za Afrika Mashariki kama 
Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Ethiopia hivyo wameungana na Red Dot 
ili waweze kukuza biashara yao zaidi.
"Tumeingia
 makubaliano na moja ya wasambazaji wakubwa wa Red Dot na tunaamini 
watatusaidia EnGenius kufikia malengo yetu ya kuwa wauzaji wakubwa wa 
bidhaa za kiteknolojia kwa Afrika Mashariki, tunafahamu kuwa ni 
wasambazaji wakubwa na atatusaidia kukuza biashara yetu," alisema Hsiao.
Na Rabi Hume, modewjiblog.com
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Red Dot Distribution akielezea jinsi ambavyo wamejipanga 
kufanya kazi na EnGenius. (Picha zote na Na Rabi Hume, modewjiblog.com)
Nae
 Mkurugenzi Mtendaji wa Red Dot Distribution, Munir Bharwani alisema 
kuwa ni ushirikiano mzuri ambao wameanza kuufanya na EnGenious na wana 
mipango mingi kuhakikisha malengo ambayo yamewekwa yanafikiwa.
"Tuna
 taraji mafanikio makubwa, Red Dot ni kampuni ya kitanzania ambayo 
inafanya kazi katika nchi za Afrika Mashariki kwahiyo tunatazamia 
ushirikiano huu utakuwa na faida," alisema Bharwani.
Meneja
 Mkuu wa Red Dot Distribution Tanzania, Rajesh Adiani akifungua halfa ya
 uzinduzi wa makubaliano kati ya Red Dot na EnGenius kwa kuelezea 
shughuli ambazo wanazifanya.
Mkurugenzi
 wa Mauzo na Masoko wa EnGenius, Alishan Zaidi akilelezea huduma ambazo 
wanazitoa za kiteknolojia na usambazaji wa vifaa vya kiteknolojia kama 
kompyuta na kamera za usalama.
Mkurugenzi
 Mtendaji wa Red Dot Distribution, Munir Bharwani na Mkuu wa Kanda wa 
EnGenius, Van Hsiao wakipongezana baada ya kuingia rasmi katika 
makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja.
Baadhi ya wageni waalikwa wakiangalia bidhaa ambazo zinatolewa na EnGenius.
Baadhi ya wageni waaliakwa waliohudhuria halfa ya makubaliano ya Red Dot Distribution na EnGenius.
 
0 Comments