VODACOM YAWALETEA WATEJA WAKE PROMOSHENI YA"JIONGEZE NA M-PAWA



Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao (kulia) akizungumza kwenye uzinduzi wa promosheni ya ‘Jiongeze na M-Pawa’ inayoendeshwa na kampuni yake ikishirikiana na Benki ya CBA, kwenye hafla iliyofanyika leo Mlimani City jijini Dar es Salaam.Ili kushiriki kwenye promosheni hiyo, mteja wa Vodacom Tanzania anatakiwa kujiwekea akiba katika akaunti yake ya M-Pawa kwenye simu yake katika kipindi cha promosheni.Jumla ya shilingi milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya promosheni hiyo na mshindi mmoja wa droo kubwa atajishindia kitita cha shilingi milioni 100.Washindi wa wiki watazawadiwa shilingi milioni 20 na washindi wa siku watazawadiwa shilingi milioni moja.Promosheni hiyo ambayo imeanza leo itadumu kwa kipindi cha wiki sita na itafikia kilele mwishoni mwa Mwezi Oktoba, 2016.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao (wa tatu kushoto) akiwa na maofisa waandamizi wa kampuni hiyo, wakionyesha mabango kwenye uzinduzi wa promosheni ya ‘Jiongeze na M-Pawa’ inayoendeshwa na kampuni yake ikishirikiana na Benki ya CBA, kwenye hafla iliyofanyika leo Mlimani City jijini Dar es Salaam.Ili kushiriki kwenye promosheni hiyo, mteja wa Vodacom Tanzania anatakiwa kujiwekea akiba katika akaunti yake ya M-Pawa kwenye simu yake katika kipindi cha promosheni.Jumla ya shilingi milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya promosheni hiyo na mshindi mmoja wa droo kubwa atajishindia kitita cha shilingi milioni 100.Washindi wa wiki watazawadiwa shilingi milioni 20 na washindi wa siku watazawadiwa shilingi milioni moja.Promosheni hiyo ambayo imeanza leo itadumu kwa kipindi cha wiki sita na itafikia kilele mwishoni mwa Mwezi Oktoba, 2016.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Ian Ferrao (kulia) na Mkurugenzi wa Mauzo na Usambazaji wa kampuni hiyo, Hassan Saleh (kushoto) wakizindua rasmi msafari wa magari kwenda mikoa mbalimbali nchini kutoa elimu juu ya promosheni ya ‘Jiongeze na M-Pawa’ inayoendeshwa na kampuni yake ikishirikiana na Benki ya CBA, kwenye hafla iliyofanyika leo Mlimani City jijini Dar es Salaam.Ili kushiriki kwenye promosheni hiyo, mteja wa Vodacom Tanzania anatakiwa kujiwekea akiba katika akaunti yake ya M-Pawa kwenye simu yake katika kipindi cha promosheni.Jumla ya shilingi milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya promosheni hiyo na mshindi mmoja wa droo kubwa atajishindia kitita cha shilingi milioni 100.Washindi wa wiki watazawadiwa shilingi milioni 20 na washindi wa siku watazawadiwa shilingi milioni moja.Promosheni hiyo ambayo imeanza leo itadumu kwa kipindi cha wiki sita na itafikia kilele mwishoni mwa Mwezi Oktoba, 2016.
Wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wakihudhuria uzinduzi wa promosheni ya ‘Jiongeze na M-Pawa’ inayoendeshwa na kampuni hiyo ikishirikiana na Benki ya CBA, kwenye hafla iliyofanyika leo Mlimani City jijini Dar es Salaam.Ili kushiriki kwenye promosheni hiyo, mteja wa Vodacom Tanzania anatakiwa kujiwekea akiba katika akaunti yake ya M-Pawa kwenye simu yake katika kipindi cha promosheni.Jumla ya shilingi milioni 300 zimetengwa kwa ajili ya promosheni hiyo na mshindi mmoja wa droo kubwa atajishindia kitita cha shilingi milioni 100.Washindi wa wiki watazawadiwa shilingi milioni 20 na washindi wa siku watazawadiwa shilingi milioni moja.Promosheni hiyo ambayo imeanza leo itadumu kwa kipindi cha wiki sita na itafikia kilele mwishoni mwa Mwezi Oktoba, 2016.

Kampuni ya Vodacom Tanzania kwa kushiriana na benki ya CBA imezindua promosheni kubwa ambayo itawawezesha watumiaji wa huduma ya M-Pawa kujishindia fedha taslimu kutoka kwenye kitita cha milioni 300 zilizotengwa kwa ajili ya promosheni hii na mshindi mmoja wa zawadi kubwa atajishindia kitita cha shilingi milioni 100.Promosheni hii inayojulikana kama ‘Jiongeze na M-Pawa’ itatoa washindi wa siku wa shilingi milioni 1/- kila mmoja,washindi wa wiki  shilingi milioni 20/- kila mmoja na wateja wapatao 200 wataongezewa mara mbili ya akiba zao walizojiwekea kwenye akaunti zao za M-Pawa kila siku.

Promosheni hii ambayo imeanza leo Agosti 31 itadumu kwa kipindi cha wiki 6 na itafikia mwishoni mwezi Oktoba ambapo itafanyika droo ya kumpata mshindi wa zawadi kubwa.Katika kipindi chote cha promosheni mabalozi wa bidhaa za Vodacom na maofisa wa kampuni watatembelea sehemu mbalimbali za Tanzania kwa ajili ya kuwaelimisha  faida za kujiwekea akiba kupitia huduma hii hususani wanaoishi maeneo ya vijijini.

Ili kushiriki kwenye promosheni anachotakiwa kufanya mteja ni kujiwekea akiba kwenye akaunti yake ya M-Pawa kwenye simu yake katika kipindi cha promosheni.Kwa kujiwekea akiba mojamoja kutawawezesha wateja kujipatia pointi za kuingia kwenye promosheni na kuwa na uwezekano wa kujishindia fedha taslimu kila siku,kila wiki na zawadi kubwa ya promosheni.Kadri mteja anavyojiwekea akiba kwenye akaunti yake ya M-Pawa ndivyo anakuwa na nafasi kubwa ya kushinda. 

Kwa mfano kwa kujiwekea akiba kati ya shilingi 1,000/-mpaka 19,000/-mteja anajipatia pointi 20,wakati akijiwekea  akiba kati ya shilingi 20,000/-mpaka shilingi 99,999/-mteja anajipatia pointi 40 na kadri anavyoweka akiba ndivyo pointi zinaongezeka  zaidi na  kuwa katika nafasi nzuri ya kushinda.

Kuweka akiba kwenye akaunti ya M-Pawa na kuwa kwenye  nafasi ya kushinda mteja anaweza kupiga  *150* 00#  kisha kwenda kwenye menu ya  M- Pawa, chagua Weka  kwenye M-pawa, weka kiasi cha fedha kisha weka namba yako ya siri ya  M-Pesa  .

Wateja watakaojishindia shilingi milioni 1/-na wale  watakaoongezewa fedha zaidi ya mara mbili ya akiba zao fedha zao zitaingizwa kwenye akaunti zao za M-Pawa moja kwa moja ambapo watafahamishwa kuwa wameshinda kupitia ujumbe mfupi wa maneno (SMS).Washindi wa wiki wa shilingi milioni 20/- na mshindi wa zawadi kubwa ya promosheni watakabidhiwa zawadi zao  na maofisa wa Vodacom watakaochaguliwa kufanya kazi hiyo kulingana na mikoa watakayotokea washindi.

Lengo kubwa la promosheni hii ni kuwahamasisha watanzania kujenga utamaduni wa kujiwekea akiba na kunufaika kwa mikopo yenye riba nafuu ya kati ya asilimia 2% hadi 5% kulingana na akiba ya mteja aliyojiwekea.”Promosheni inawakumbusha watanzania kuwa kuweka akiba kwenye M-Pawa ni chaguo la busara hususani kwa wajasiriamali kwa kuwa inawezesha kupata mikopo nafuu yenye riba ndogo”.amesema Ian Ferrao,Mkurugenzi mtendaji wa Vodacom Tanzania .

“Huduma ya M-Pawa ni akaunti ya benki kwenye ncha ya kidole chako ambayo imebuniwa kuboresha maisha ya wateja!Zaidi ya watanzania milioni 4.8 wanaendelea kufurahia huduma hii na natoa wito kwa watanzania wengi wajiunge zaidi na kufurahia huduma hii ya M-Pawa.Unavyojiwekea akiba zaidi ndivyo kiwango cha kukopa kinavyoongezeka”.Alisisitiza Ferrao.

No comments:

Post a Comment

Pages