NBC Yazindua Klabu ya Biashara mjini Kahama






Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC, William Kallaghe (kushoto), akizungumza wakati wa uzinduzi rasmi wa Klabu ya Biashara ya benki hiyo mjini Kahama, Shinyanga jana. Klabu hiyo imeanzishwa kusaidia mahitaji ya wateja wafanyabiashara wadogo na wa kati. Katikati ni mmoja wa wateja, Salum Selemani na Joshua John (kulia), Ofisa Masoko wa Chama cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo (TCCIA) kutoka ofisi ya Mwanza.

Meneja Mahusiano wa Benki ya NBC, William Kallaghe (kushoto), akizungumza na baadhi ya wafanyabiashara wa mjini Kahama, katika semina iliyoandaliwa kabla ya uzinduzi rasmi wa Klabu ya Biashara ya NBC hiyo iliyoanzishwa kusaidia mahitaji ya wateja wafanyabiashara wadogo na wa kati. Hafla ya uzinduzi ilifanyika mjiini Kahama, Shinyanga jana.

Meneja wa Kanda wa NBC, Daudi Mfalla (kulia), akizungumza wakati akizungumza katika hafla ya uzinduzi rasmi wa Klabu ya Biashara ya NBC iliyoanzishwa kusaidia mahitaji ya wateja wafanyabiashara wadogo na wa kati. Kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Wafanyabiashara wadogo na wakati wa NBC, Evance Luhimbo.

Baadhi ya wateja wa NBC mjini Kahama waliohudhuria uzinduzi wa B-Club ya benki hiyo, wakijipiga picha ‘selfie’ pamoja na bango lenye picha inayoonyesha kilele cha Mlima Kilimanjaro ikiwa ni baadhi ya shamrashara zilizopamba uzinduzi huo.

Wafanyakazi wa NBC tawi la Kahama wakipozi kwa katika hafla hiyo.

Wasanii wakionyesha umahiri wao kucheza ngoma ya kadete ya kabila la wasukuma katika hafla ya uzinduzi wa B-Club mjini Kahama, Shinyanga jana.

No comments:

Post a Comment

Pages