BENKI YA TIB YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA KWA KUENDELEA KUTOA HUDUMA ZENYE UBUNIFU





BENKI ya biashara inayomilikiwa na Serikali ya Tanzania Investment Bank (TIB) inaendelea kutoa huduma mbalimbali za kibenki zenye ubunifu wa hali ya juu ili kufikia dira ya kuwa benki ambayo ni chaguo la wateja.


Hayo yamesemwa ka Mkurugenzi mtendaji wa benki ya TIB, Frank Nyabundege wakati akizungumza na wateja wa benki ya TIB waliofika katika tawi la Samora jijini Dar es Salaam leo. Amesema kuwa benki hiyo inatoa huduma za TIB mobile, Utoaji wa bure wa dhamana za kibenki, sms alert, Premier banking, uboreshaji wa kazi za ATM, kutua huduma masaa 24 ya katika tawi la bandari, huduma za malipo ya kodo kirahisi pamoja na JIPANGE Plan.


Amesema kuwa "Huu ni mwaka ni waka wetu wa pili tangia kupata kibali cha kutoa huduma za kibenki na kuendelea kujenga uwezo wa kuwapa wateja huduma za kipekee."


Amesema kuwa hudum nzuri kwa wateja ndio kipaumbele katika maendeleo ya benki hiyo.



Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya TIB, Frank Mwabundege akihudumia wateja ikiwa ni wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka mwezi Oktoba duniani kote.

Wafanyakazi wa benki ya TIB wakiwahudumia wateja wa waliofika katika benki hiyo jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka Oktoba duniani kote.

Mteja wa benki ya TIB, Irene Kiwia akizungumza na Michuzi TV jijini Dar es Salaam leo wakati alipofika katika benki ya TIB jijini Dar es Salaam wakati wa kuwashukuru wateja wa benki hiyo.

Mkuu wa masoko na mahusiano wa Benki ya TIB, Theresia Soka akizungumza na wateja pamoja na wafanyakazi wa benki ya TIB waliofika katika benki hiyo jijini Dar es Salaam leo.
Amewashukuru wateja wa benki hiyo kufka katika taw la Samora kwaajili ya kusheherekea pamoja wiki ya huduma kwa wateja pamoja na kuwaomba kutoa maoni yao ili kwenye mapungufu wajirekebisha.


Baadhi ya wateja na wafanyakazi wa benki ya TIB wakiwa katika hafla fupi ya kuwashukuru wateja wao katika wiki ya huduma kwa wateja.


Mteja wa benki ya TIB, Irene Kiwia pamoja na wateja wengine wakishirikiana kukata keki kwaajili ya kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila mwaka Oktoba.

Mkuu wa masoko na mahusiano wa Benki ya TIB, Theresia Soka akikatakata keki kwaajili ya kulishwa wateja wa benki ya TIB jijini Dar es Salaam leo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya TIB, Frank Nyabundege akimlisha keki Mteja wa benki ya TIB, Irene Kiwia ikiwa ni kuadhmisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila wiki ya kwanza ya Oktoba kila mwaka.
Kushoto ni Mfanyakazi mstaafu wa benki ya TIB akilishwa keki jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja.

Baadhi ya wateja wa benki ya TIB wakilishwa keki jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kuadhimisha wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila wiki ya kwanza ya Oktoba kila mwaka.

Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya TIB, Adolphina William akimpa zawadi mteja wa benki ya TIB kutoka jijini Mbeya na mmiliki wa Kampuni ya GDM Ltd, Grivas Mwangoka.

Mkurugenzi wa biashara wa benki ya TIB, Mwallu Mwachang'a akizungumza na wateja pamoja na kuwashukuru kufuka katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika Kila Oktoba kila mwaka duniani kote.

Meneja wa tawi la benki ya TIB tawi la Samora, Philipo Pilla akiwashukuru wateja wa wa benki ya TIB na waendelee kufurahia huduma za benki ya TIB.

No comments:

Post a Comment

Pages