MSHINDI WA SHILINGI MILIONI 10 KUPITIA PROMOSHENI YA JAYMILLIONS YA VODACOM AKABIDHIWA KITITA CHAKE.


 Mkuu wa Vodacom Tanzania  kanda ya ziwa Dominician Mkama(kushoto)akimkabidhi kitita  cha shilingi Milioni 10/- James Mangu ambaye ni mjasiliamali mkazi wa Magu mkoa wa Mwanza,alizojishindia kupitia promosheni ya JayMillions  inayoendeshwa na kampuni hiyo, wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika tawi la Benki ya mkoani humo leo.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay au AUTO kwenda 15544. 
 Mshindi wa kitita cha Shilingi Milioni 10/- kupitia promosheni ya JayMillions  inayoendeshwa na Vodacom Tanzania, James Mangu ambaye ni mjasiliamali mkazi wa Magu mkoa wa Mwanza,akiwa ameshikilia kitita chake alichojishindia kupitia promosheni ya JayMillions  inayoendeshwa na kampuni hiyo, wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika tawi la Benki ya mkoani humo leo.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay au AUTO kwenda 15544.
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Kenyatta Mwanza, Martin Rajabu(kulia)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa kumkabidhi kitita  cha shilingi Milioni 10/- James Mangu ambaye ni mjasiliamali mkazi wa Magu mkoa wa Mwanza,alizojishindia kupitia promosheni ya JayMillions  inayoendeshwa na Vodacom Tanzania,hafla hiyo ilifanyika katika tawi la Benki hiyo mkoani humo leo anaeshuhudia kushoto ni Mkuu wa Vodacom Tanzania  kanda ya ziwa Dominician Mkama.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay au AUTO kwenda 15544.

 Mkuu wa Vodacom Tanzania  kanda ya ziwa Dominician Mkama(kushoto)akimkabidhi kitita  cha shilingi Milioni 10/- James Mangu ambaye ni mjasiliamali mkazi wa Magu mkoa wa Mwanza,alizojishindia kupitia promosheni ya JayMillions  inayoendeshwa na kampuni hiyo, wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika tawi la Benki ya mkoani humo leo.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay au AUTO kwenda 15544. 
 Mshindi wa kitita cha Shilingi Milioni 10/- kupitia promosheni ya JayMillions  inayoendeshwa na Vodacom Tanzania, James Mangu ambaye ni mjasiliamali mkazi wa Magu mkoa wa Mwanza,akiwa ameshikilia kitita chake alichojishindia kupitia promosheni ya JayMillions  inayoendeshwa na kampuni hiyo, wakati wa hafla fupi iliyofanyika katika tawi la Benki ya mkoani humo leo.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay au AUTO kwenda 15544.
Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Kenyatta Mwanza, Martin Rajabu(kulia)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa kumkabidhi kitita  cha shilingi Milioni 10/- James Mangu ambaye ni mjasiliamali mkazi wa Magu mkoa wa Mwanza,alizojishindia kupitia promosheni ya JayMillions  inayoendeshwa na Vodacom Tanzania,hafla hiyo ilifanyika katika tawi la Benki hiyo mkoani humo leo anaeshuhudia kushoto ni Mkuu wa Vodacom Tanzania  kanda ya ziwa Dominician Mkama.Ili mteja kujua kama ameshinda anatakiwa kutuma neno Jay au AUTO kwenda 15544.


MSHINDI WA SHILINGI MILIONI 10 KUPITIA PROMOSHENI YA JAYMILLIONS YA VODACOM AKABIDHIWA KITITA CHAKE.

Mkazi wa wilaya ya Magu mkoani Mwanza anayejishughulisha na ujasiriamali James Mangu leo amekabidhiwa kitita cha milioni 10/-alizojishindia kupitia promosheni ya Jaymillions inayoendeshwa na Vodacom Tanzania katika hafla iliyofanyika katika tawi la Benki ya CRDB tawi la  Mwanza Mama jijini Mwanza.

Mangu alikabidhiwa fedha zake na Mkuu wa kanda ya ziwa wa Vodacom Tanzania,Dominick Mkama akiwa na Meneja wa CRDB wa tawi hilo Bw.………mbele ya waandishi wa habari.

Akiongea muda mfupi baada ya kupokea fedha zake za ushindi Mangu alisema kuwa siku ya leo itabaki kwenye kumbumbukumbu za historia kwa kuwa ndoto aliyokuwa nayo muda mrefu kupanua biashara yake imetimia.“Vodacom kupitia promosheni hii wamefanya ndoto yangu ya kuwa mfanyabiashara mkubwa kutimia kwa kutumia shilingi mia tatu tu na kuandika neno  JAY kwenda namba 15544”.Alisema Mangu kwa furaha.James Mangu amewaomba Watanzania kutambua mchango mkubwa unaofanywa na Kampuni hiyo nchini katika kujenga na kuimarisha maisha ya Watanzania na wateja wake kwa ujumla.

"Promosheni ya Jaymillions naona inalenga kuwakomboa kimaisha watanzania hususani wenye kipato cha chini hasa  wajasiriamali wadogo wadogo kama vile; wamachinga, mama ntilie, na wazee wastaafu ambapo kwa kiasi kikubwa  wanahitaji msaada ili kujiendeleza kiuchumi na kuinua hali za maisha yao.  Promosheni ya Jaymillions inayoendelea ikiwa katika wiki ya sita na ambayo itadumu kwa muda wa siku 100  itaendelea kuleta faraja na mafanikio kwa wateja wa Vodacom kwa kuweza kujinasua katika hali duni ya maisha na maisha kuwa murua.


  Hadi kufikia leo ni Sh. 134m/- pekee zilizokwisha kuchukuliwa na Uwezo Madengenya na washindi wengine wawili – Hyness Petro Kanumba kutoka Rukwa na James Mangu (Mwanza) – wa Sh. 10m/- na milioni 11m/- zimekwenda kwa – Chiliphod Wanjala (Mwanza), Janeth Nganyange (Njombe), Evarista A (Mwanza), Stanley Bagashe (Shinyanga), Ramadhani H. Maulid (Dodoma) na  Lucas Masegese (Shinyanga),Ayubu Makonde(Mbeya), Hyasinti Mlowe(Njombe), Florian Gwayu(Arusha), Modesta Milanzi(Ruvuma), Nobert Minungu(Dodoma), Busolo Swaleh(Arusha), Claudia Simon Mapunda(Dar es Salaam)  na Gerald Shao (Kilimanjaro)– wa Sh. 1m.

  Mkuu wa kanda ya ziwa wa Vodacom Tanzania Dominick Mkama, akiongea katika hafla hiyo alimpongeza mshindi huyo na kusema kwamba fedha hizo zimeenda kwa mshindi sahihi kwani mshindi huyo ana malengo mazuri ya matumizi ya fedha zake kwa  kupanua shughuli zake za biashara  kwa ajili ya kuinua kipato cha familia yake na wananchi wa kanda hii.

 Pia aliwahimiza wateja wote kuchangamkia promosheni ya Jaymillions ili wajishindie mamilioni ya fedha kwa kuhakikisha wanatuma neno JAY kwenda namba 15544 ili kutopoteza bahati zao  za kushinda.Aliitaja njia nyingine ya kushinda kuwa ni kutuma neno AUTO kwenda namba 15544 iwapo simu haina fedha ambapo  mteja akiweka fedha anakatwa shilingi 300/-tu.

Kwa upande wake Meneja wa CRDB Martin Rajabu alimpongeza  mshindi na kumshauri kuwa watampa muongozo bora na ndoto yake ya kuwa mfanyabiashara mkubwa itatimia na kumsisitiza kutembelea  tawi la benki hiyo wakati wowote kwa ajili ya kupata ushauri jinsi gani ya kukuza biashara zake kwa kuwa benki hiyo ina huduma mbalimbali za kuwawezesha wafanyabiashara.Pia aliipongeza Vodacom kwa kubuni promosheni za aina hii zenye mwelekeo chanya wa kuinua maisha ya wateja wake na wananchi kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment

Pages